Psalms 3

Sala Ya Asubuhi Ya Kuomba Msaada

Zaburi Ya Daudi Alipomkimbia Mwanawe Absalomu.


1 aEe Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi!
Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

2 bWengi wanasema juu yangu,
“Mungu hatamwokoa.”


3 cLakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote;
umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

4 dNinamlilia Bwana kwa sauti kuu,
naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.


5 eNinajilaza na kupata usingizi;
naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.

6 fSitaogopa makumi elfu ya adui,
wanaojipanga dhidi yangu kila upande.


7 gEe Bwana, amka!
Niokoe, Ee Mungu wangu!
Wapige adui zangu wote kwenye taya,
vunja meno ya waovu.


8 hKwa maana wokovu watoka kwa Bwana.
Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Copyright information for SwhKC